ABOUT US


Uwanja wa vijana unashughurika na kutengeneza ajira ,kununua na,kuuza ajira,mawazo ya biashara au miradi pamoja na kuwawezesha vijana na watu wengine kiuchumi,tunawatoa watu kimaisha kwa pale anapo taka kufika na  kuzitafuta fursa,na kuandaa mitego mbalimbali ya kuzinasa fursa mikoa yote ya Tanzania,pia tunawasaidia wanavyuo jinsi ya kutumia fedha wanazo zipata, pia tunatoa elimu ya fedha na matumizi ya mda,pamoja na kuwasaidia watu wote wanao karibia kustaafu kazi ili waweze kuishi maisha mazuri yasiyo na mapresha yanayoweza kusababisha umauti kabla ya wakati

Uwanja wa vijana umepata ufumbuzi wa mkwamo na changamoto zote walizonazo au wanazokabiliana nazo vijana wa kitanzania baadhi ya matatizo (changamoto hizo ni pamoja na maswala ya kiuchumi, umaskini, Ajira,mahusiano na ndoa  pia uwanja wa vijana utafanya kazi ya kuwafungua vijana vifungo mbalimbali walivyo jifunga wenyewe au kufungwa na viongozi wa dini\siasa;wazazi/vyeti vyao/mitandao/mali za wazazi/uzuri wao/dini zao/mitizamo na misimamo yao/mila na desturi zao nk. Uwanja wa vijana utahakikisha swala la uadui uliopo kati ya vijana na wazee unaondoka huo wa kwamba wazee hawawezi kuwaachia nafasi za kazi kwakuwa vijana hawajatulia na vijana wanasema  wazee wamepitwa na wakati na pia hawajasoma, pamoja na swala la kuilaumu serikali  yao  kuwa haiwasaidii au ndugu na jamaa zao bila kujua  kuwa chanzo cha  matatizo hayo ni wao  wenyewe vijana, Uwanja wa vijana pia utafanya kazi ya kufufua uchumi kuanzia ngazi ya mtu mmoja mmoja.ngazi ya familia, ukoo, kijiji, kata, wilaya, mkoa hadi taifa.                                                                                                                           

2 comments: